Zaidi ya wanafunzi 200 wa shule ya msingi Kingolwira wagundulika kuwa na magonjwa ya meno na fizi

Zaidi ya wanafunzi 200 wa  shule ya msingi KINGOLWIRA katika manispaa  ya morogoro wamegundulika kuwa na matatizo ya kinywa na meno na  baada ya madaktari wa afya ya kinywa katika hospitali ya mkoa wamorogoro kufanya  uchunguzi na kuwasafisha meno wanafunzi.

Akizungumza wakati wa zoezi la utoaji wa huduma ya afya ya kinywa na meno katika shule ya msingi KIGOLWIRA na katika kituo cha kulea wazee wasiojiweza cha fungafunga mjini morogoro  Daktari wa meno Samson Tarimo amesema baada ya kufanya uchunguzi na kuwasafisha meno wamebaini idadi kubwa ya wanafunzi meno yao yameoza  ambapo amewataka wazazi kuwapeleka watoto hospitali kw amatibabu zaidi.
 
Kwa upande wao baadhi ya wanafunzi na wazee waliopata huduma hiyo wameshukuru  madaktari ambapo wameeleza  walikuwa wakisumbuliwa na tatizo la meno kwa muda mrefu  bila kupata ufumbuzina kuiomba serikali kuwezesha juhudi zilizoanzishwa na madaktari hao kuwa endelevu.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo