Walimu wa Shule ya Msingi Mafizi iliyopo Kisarawe, Pwani wako hatarini kutokana na vyoo wanavyovitumia kudidimia ambapo kutokana na hali hiyo wamelazimika kujisaidia vichakani na wengine katika vyoo vya Zahanati.
Mwalimu Mkuu wa Shule hiyo, Manyama Philipo amesema; “Kwa kweli sasa tuna changamoto ya vyoo.. mvua hizi zinazonyesha vyoo vyote vimetitia.. tuna hali mbaya”
Mmoja wa Walimu wa Shuleni hapo, Eveline Munisi amesema kutokana na jinsi hali ilivyo walimu wa kike wanalazimika kwenda porini wakiwa na majembe kwa ajili ya kujisaidia.