Hospitali ya Taifa ya Muhimbili inalalamikiwa kuwa na unyanyapaa kwa wagonjwa wanaofika hapo ili kupata huduma za afya kutokana na madaktari na manezi kuwa na kauli mbaya na zisizofaa kwa wagonjwa.
Baadhi ya wagonjwa wanaopata huduma katika hospitali hiyo inayotegemewa na Taifa ni tia maji tiamaji kwa vile kwa vile ni mbovu na haifai na kusababisha kuishushia hadhihospitali hiyo.
Katika hospitali hiyo wodi inayolalamkiwa zaidi ni ile ya mifupa MOI kwa kudaiwa kujaza watu wengi hadi kulala chini, mashuka hayabadilishwi kwa wakati na pia madaktari hawapiti kwa muda uliopangwa.
“Hii hospitali ni bure kabisa nimemleta mgonjwa hapa hali ikiwa mbaya kabisa,lakini daktari hakuwa na muda zaidi ya kuuliza nimejipanga vipi ili mgonjwa wangu ahudumiwe vizuri, hadi nilipompa pesa ndipo mgonjwa wangu akatibiwa, inasikitisha”.
Aliongeza kuwa hata alipomfikisha mgonjwa wake kitengo cha MOI wauguzi waliokuwepo zamu siku hiyo hawakumpokea wala kumjali mgonjwa na kuendelea na maongezi.