Rais Jakaya Kikwete amesema serikali inatafuta fedha za kujenga nyumba
468 mpya za kisasa na kukarabati nyumba zilizoezuliwa na upepo katika
eneo la Mwakata huko Kahama mkoani Shinyanga pamoja na kuendelea
kuhudumia waathrika wote kwa chakula, malazi na dawa hadi watakapopata
makazi bora ya kudumu.

Rais Jakaya Mrisho Kikwete akizungumza na kuwafariji waathirika wa Mvua ya Mawe,iliyonyesha hivi karibuni katika Kijiji cha Mwakata,Wilayani Kahama Mkoa wa Shinyanga,leo Machi 12,2015.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akizungumza na kuwafariji waathirika wa Mvua ya Mawe,iliyonyesha hivi karibuni katika Kijiji cha Mwakata,Wilayani Kahama Mkoa wa Shinyanga,leo Machi 12,2015.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akizungumza na kuwafariji waathirika wa Mvua ya Mawe,iliyonyesha hivi karibuni katika Kijiji cha Mwakata,Wilayani Kahama Mkoa wa Shinyanga,leo Machi 12,2015.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akizungumza na kuwafariji waathirika wa Mvua ya Mawe,iliyonyesha hivi karibuni katika Kijiji cha Mwakata,Wilayani Kahama Mkoa wa Shinyanga,leo Machi 12,2015.
Rais Jakaya Kikwete
amesema Serikali itajenga nyumba 403 ambazo zimebomolewa na mvua kubwa
iliyonyesha wiki iliyopita katika kijiji cha Mwakata wilayani Kahama na
kusababisha watu 649 kukosa mahali pa kuishi.
Kauli hiyo aliitoa jana kwenye kijiji
cha Mwakata baada ya kutembelea eneo lililoathiriwa na mvua hiyo na
kujionea maisha duni wanayoishi watu hao.
Akizungumza na wananchi waliohudhuria
mkutano wake Rais Kikwete alisema Serikali iko pamoja na wananchi hao na
itahakikisha makazi yao yanarejea katika hali yake ya kawaida kwa
kuwajengea nyumba hizo.
Pia, Rais Kikwete aliagiza Jeshi la Kujenga Taifa(JKT)
wajenge nyumba hizo bila kupitia mkandarasi yeyote kama vile ulivyo
ujenzi wa Serikali kwa kuwa ujenzi wa jeshi unaisha kwa muda mfupi na
hakuna uchakachuaji
Aliwataka viongozi mkoani Shinyanga
kuhakikisha ujenzi huo hautangazwi na kuagiza JKT kwenda kwenye eneo
hilo kufanya tathmini ya ujenzi huo ili uanze mara moja.
Rais Kikwete aliwatoa wasiwasi wananchi
wa Mwakata waliokumbwa na tatizo hilo kwamba Serikali itahakikisha wote
wamepata chakula hadi mwisho watakapolima na kupata mavuno na tukio hilo
wasilihusishe na imani za kishirikina.
Alisema mvua hizo ni za kawaida ambazo
hutokana na mabadiliko ya tabia ya nchi na si ushirikina hivyo aliwataka
wananchi hao waendelee kuwa na hisia hizo lakini wasilichukulie kwa
uzito swala la ushirikina wakatafuta mchawi wa mvua hiyo
Awali, Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Ally Rufunga
alimwambia Rais Kikwete kwamba mvua hiyo licha ya kuua watu 47 pia
imeharibu mazao hekari 2,332 pamoja na visima 53 vya maji ya kunywa.
Rufunga alisema mpaka kufikia sasa
wahisani mbalimbali wamechangia kwenye tukio hilo Sh64 milioni pamoja na
tani 63 za unga wa sembe pamoja na mahitaji mbalimbali ya kibinadamu
yakiwamo mabati zaidi ya 1,000
