RAIS KIKWETE AFIKA KAHAMA KUJIONEA MADHARA YA MAFURIKO NA KULIAGIZA JESHI

Rais Jakaya Kikwete amesema serikali inatafuta fedha za kujenga nyumba 468 mpya za kisasa na kukarabati nyumba zilizoezuliwa na upepo katika eneo la Mwakata huko Kahama mkoani Shinyanga pamoja na kuendelea kuhudumia waathrika wote kwa chakula, malazi na dawa hadi watakapopata makazi bora ya kudumu.
jkm1
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akizungumza na kuwafariji waathirika wa Mvua ya Mawe,iliyonyesha hivi karibuni katika Kijiji cha Mwakata,Wilayani Kahama Mkoa wa Shinyanga,leo Machi 12,2015. jkm2
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akizungumza na kuwafariji waathirika wa Mvua ya Mawe,iliyonyesha hivi karibuni katika Kijiji cha Mwakata,Wilayani Kahama Mkoa wa Shinyanga,leo Machi 12,2015.

Rais Jakaya Kikwete amesema Serikali itajenga nyumba 403 ambazo zimebomolewa na mvua kubwa iliyonyesha wiki iliyopita katika kijiji cha Mwakata wilayani Kahama na kusababisha watu 649 kukosa mahali pa kuishi.
Kauli hiyo aliitoa jana kwenye kijiji cha Mwakata baada ya kutembelea eneo lililoathiriwa na mvua hiyo na kujionea maisha duni wanayoishi watu hao.
Akizungumza na wananchi waliohudhuria mkutano wake Rais Kikwete alisema Serikali iko pamoja na wananchi hao na itahakikisha makazi yao yanarejea katika hali yake ya kawaida kwa kuwajengea nyumba hizo.
Pia, Rais Kikwete aliagiza Jeshi la Kujenga Taifa(JKT) wajenge nyumba hizo bila kupitia mkandarasi yeyote kama vile ulivyo ujenzi wa Serikali kwa kuwa ujenzi wa jeshi unaisha kwa muda mfupi na hakuna uchakachuaji
Aliwataka viongozi mkoani Shinyanga kuhakikisha ujenzi huo hautangazwi na kuagiza JKT kwenda kwenye eneo hilo kufanya tathmini ya ujenzi huo ili uanze mara moja.
Rais Kikwete aliwatoa wasiwasi wananchi wa Mwakata waliokumbwa na tatizo hilo kwamba Serikali itahakikisha wote wamepata chakula hadi mwisho watakapolima na kupata mavuno na tukio hilo wasilihusishe na imani za kishirikina.

Alisema mvua hizo ni za kawaida ambazo hutokana na mabadiliko ya tabia ya nchi na si ushirikina hivyo aliwataka wananchi hao waendelee kuwa na hisia hizo lakini wasilichukulie kwa uzito swala la ushirikina wakatafuta mchawi wa mvua hiyo

Awali, Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Ally Rufunga alimwambia Rais Kikwete kwamba mvua hiyo licha ya kuua watu 47 pia imeharibu mazao hekari 2,332 pamoja na visima 53 vya maji ya kunywa.

Rufunga alisema mpaka kufikia sasa wahisani mbalimbali wamechangia kwenye tukio hilo Sh64 milioni pamoja na tani 63 za unga wa sembe pamoja na mahitaji mbalimbali ya kibinadamu yakiwamo mabati zaidi ya 1,000


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo