MAUAJI TENA: Mfanya biashara Arusha adaiwa kumuua rafiki yake

MFANYABIASHARA maarufu wa madini ya tanzanite jijini Arusha, Felix Mmasi (41) anashikiliwa na Jeshi la Polisi mkoani Arusha akituhumiwa kumpiga risasi kwa kutumia silaha aina ya bastola mtu anayedaiwa kuwa ni rafiki yake na kumsababishia umauti. 

Tukio hilo limethibitishwa na Kamanda wa Polisi mkoani Arusha, Liberatus Sabas alipoulizwa na mwandishi wa gazeti hili juu ya kuwepo kwa tukio hilo. 

Sabas alikiri Polisi kumshikilia mtuhumiwa huyo, lakini alisema taarifa rasmi ya tukio hilo atazitoa leo kwa waandishi wa habari mara baada ya kuchukua maelezo kwa mtuhumiwa. 

Katika Kituo Kikuu cha Polisi, wafanyabiashara wa madini na watu wengine walimiminika kumshuhudia mwenzao, huku wengine wakionekana kutafuta njia za kutoa kila aina ya msaada kwa mwenzao. 


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo