Hukumu ya kifo kwa watuhumiwa wa mauaji ya albino yapokelewa kwa mitazamo tofauti

Hukumu ya kifo kwa watuhumiwa wa mauaji ya watu  wenye ulemavu wa ngozi iliyotolewa  na mahakama  kuu imeibua hamasa na mitazamo tofauti kwa wananchi  ambao pamoja na kupongeza hatua hiyo wamesema  wanachosubiri sasa  ni  kuona  ngazi  zinazohusika  zikitekeleza  hukumu hiyo.

Wananchi hao wamesema ili adhabu hiyo iweze kuwa na  tija na kuwa fundisho kwa  wengine ni vyema utelezaji wa hukumu iliyotolewa ufanyika haraka na  jamii ione huku wengine wakitaka kesi zinazohusiana  na mauaji ya albino zitenganishwe na kesi zingine  ili zisichukue  muda mrefu. 
 
Katika hatua Bi.Ester Mahawe ambaye ni mkurugenzi  wa  shule ya Intel School ya mkoani arusha   amejitolea kuwasomesha watoto wawili wenye ulemavu  wa ngozi ambao mdogo wao aliuawa hivi karibuni   huko geita.
 
Akitangaza azima yake hiyo Bi.Ester amesema baada  ya kutafakari kwa muda amebaini kuwa anachoweza  kusaidia ni kuwalea na kuwasomesha watoto hao,Shija Bahati (11) na Aseri Bahati (2) kuanzia  elimu ya awali hadi darasa  saba.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo