Chama cha walemavu wa ngozi mkoa wa Mwanza kimepongeza hotuba ya Rais Kikwete

Chama cha walemavu wa ngozi mkoa wa Mwanza kimepongeza hotuba ya rais Mhe.Dr.Jakaya Mrisho Kikwete jana alipolihutubia taifa kupitia vyombo vya habari akilaani ukatili dhidi ya mauaji ya walemavu wa ngozi hapa nchini huku akivitaka vyombo vya kisheria kuwasaka hadi kuwakamata watuhumiwa ili wafikishwe mahakamani na kupewa adhabu inayo wa sitahili kwa lengo la kudhi biti mauaji ya albino yanayodhalilisha na kufedhehesha taifa la Tanzania ambalo linasifika umoja wa mataifa kuwa kisiwa cha amani.

Aidha rais Mhe.Dr.Jakaya Mrisho Kikwete katika hotuba yake alisisitiza kuimalisha ulinzi hapa nchini na kukubali kukutana na viongozi wa chama cha walemavu wa ngozi wiki ijayo kwa lengo la kutafuta ufumbuzi wa kumaliza tatizo la mauaji ya albino ambapo mwenyekiti wa chama cha albino mkoa wa Mwanza Bw.Alfred Kapole amempongeza rais kwa kulaani mauaji ya albino na kusema kwamba endapo watendaji wa serikali wakitekeleza agizo rais ukatili dhidi ya walemavu wa ngozi utapungua au kukomeshwa kabisa. 
 
Wakati huohuo balozi wa marekani hapa nchini Mh.Mark Chidless amemtumia salam za lambilambi mgonjwa Bi.Ester Jonas aliyejeruhiwa vibaya na watu wasiojulikana hali iliyoradhim  kulazwa katika hospitali ya rufaa Bugando jijini Mwanza na kumpa pole kwa kupoteza mtoto wake kipenzi Yohana Bahati mwenye umri wa mwaka mmoja aliyetekwa nyara na wahalifu kisha wakamuuwa na kutoweka na baadhi ya viungo vyake ikiwemo mikono na miguu ambapo salam hizo zimewasilishwa na afisa usitawi wa jamii wa shirika la kutetea haki za watu wenye ulemavu wa ngozi Tanzania Under the same sun Bi.Ester Rwela kwa niaba ya mkurugenzi wa shirika Vick Ntetema na kusema kwamba balozi wa marekani amesikitishwa sana na uhalifu unaotendeka dhidi ya walemavu wa ngozi na kuitaka serikali ya Tanzania kuwachukulia hatuua za kisheria watuhumiwa wa mauaji ya walemavu wa ngozi.
 
Wakiwashukuru wasamalia wema wa ndani na nje ya nchi Bi.Ester Jonas na mama yake mzazi Bi.Tabu Maganiko baada ya kupokea msaada wa fedha kiasi cha shilingi milioni moja kutoka ITV, Radio One zilizotolewa na mfuko wa hifadhi ya jamii GEPF ambapo katika kipindi cha wiki mbili zaidi ya shilingi milioni saba zimepatikana kutokana na misaada ya watu mbalimbali wa ndani na nje ya nchi huku wakiomba mashirika na taasisi kuwasaidia kulea watoto wawili wa Ester Jonas walemavu wa ngozi ambao wanaishi kwa hofu kubwa hoko kijijini baada ya mdogo wao kuuwa wa kinyama.
 


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo