Na: Sylvester Onesmo wa Jeshi la Polisi Dodoma
Watu
wawili wamefariki dunia papo hapo katika ajali ya Basi kugongana na Lori
ajali iliyotokea tarehe 19/02/2015 majira ya saa saba mchana
huko eneo la Vikonje Kata ya Mtumba Barabara ya Dodoma – Morogoro.
Kamanda
wa Polisi Mkoa wa Dodoma Kamishina Msaidizi Mwandamizi wa Polisi DAVID
MISIME – SACP amesema ajali hiyo imehusisha Basi lenye namba za usajili
T. 663 AXL aina ya SCANIA Kampuni ya KIDIA ONE lililokuwa litokea Dar es
Salaam kwenda Mwanza likiendeshwa na ADAM s/o ROBERT, 38yrs, kabila
Mnyaturu, mkazi wa Tegeta Dar es Salaam, liligongana uso kwa uso na Lori
namba T.469 CFG Scania lenye Tellar T. 756 AZX.
Kamanda
MISIME amewataja waliofariki dunia kuwa ni FADHILI S/O HAMIDU SAIDI
miaka 36, Kabila Msukuma ambaye ni dereva wa Lori na utingo wa Bus
aliyehafamika kwa jina la CHOGO S/O CHIGUNDA, miaka 30, Kabila Muha wote
wakazi wa Dar es Salaam.
Majeruhi
katika ajali hiyo ni 45 kati yao 34 ni wanaume na 11 ni wanawake;
wengine wametibiwa na kuruhusiwa. Waliolazwa ni 24 kati yao wanaume ni
17 na wanawake ni 7.
Kamanda
MISIME amesema chanzo cha ajali ni dereva wa Bus Kushindwa kuchukua
tahadhali wakati wa kulipita gari lingine “over take”, na kusababisha
ajali hiyo.
Aidha
Kamanda MISIME ametoa wito kwa madereva kuwa na udereva wenye tahadhali
na kuzingatia sheria za usalama barabarani, kwani dereva huyu wa basi
angezingatia hilo ajali hii haingetokea na hatakama ingetokea madhara
yake hayangekua makubwa kiasi hicho.