Mwenye nyumba kafanya utapeli kwa wapangaji zaidi ya kumi DAR, Ishu yafika mahakamani

Hekaheka hii inatoka Kinondoni Dar, ishu ni kesi ambayo tayari imefika kituo cha Polisi Oysterbay ambapo mwenye nyumba mmoja amekuwa akichukua kodi kwa wapangaji wengi ambao wanaletwa kwa nyakati tofauti halafu anawadanganya kwamba kuna watu wanakaribia kuhama vyumba vitakuwepo kitu ambacho sio kweli.

Baada ya wapangaji hao kushtuka kwamba wanafanyiwa utapeli mmoja wao alimkamata mwenye nyumba huyo na kumpeleka Kituoni hapo, amekaa kwa zaidi ya wiki moja huku wakipewa taarifa na askari kwamba madeni ya wapangaji hao inakaribia milioni 40 na mwenye nyumba huyo hana hela kuwalipa wote wanaomdai.
Nyumba Kino
Picha hii imewekwa na Geah Habib katika ukurasa wake Instagram, kinachoonekana hapo ni ‘mwenye nyumba’ huyo, nyumba yake na mkataba wa mpangaji mmoja aliyetapeliwa.

Majirani wa nyumba hiyo wamesema kuwa hiyo nyumba ni ya urithi ambayo ndugu wamegawana vyumba na kupangisha lakini huyu amekuwa na tabia ya utapeli na pia ana tabia ya kuwaibia wapangaji wake ambao tayari wanaishi hapo, anawapa funguo moja moja za milango halafu nyingine anabaki nazo, wakiwa hawapo anafungua na kuwaibia.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo