MWALIMU WA SEKONDARI YA KIBASILA AAMUA KUKAA NA KINYESI, MENDE NA FUNZA NDANI KWA MIAKA MIWILI

tooopHalmashauri ya Manispaa ya Temeke imeingilia kati tukio la mwalimu wa Sekondari ya Kibasila, Gaudensia Albert kukaa na kinyesi ,mende na funza ndani kwa muda wa miaka miwili na kutaka kumchukulia hatua.

Ofisa Afya Manispaa ya Temeke Willium Mihemu alisema kwa sasa yupo kwenye mikakati ya kujiandaa kushirikiana na  na askari polisi kumchukulia hatua mwalimu huyo anayefundisha masomo ya sayansi hapo shuleni.

Leo sisi na Polisi tutaungana ili kwenda kumkamata,kwani kwa hali ya kawaida inaonekana mwalimu huyo hana akili timamu“-Mihemu.

Kwa upande wa mwenye nyumba Ruben Shayo ambaye wanaishi eneo la Yombo Visiwani alisema kuwa licha ya kufanya tukio hilo kwa miaka miwili mfululizo lakini bado alimruhusu kuendelea kuishi ndani ya nyumba yake na kumtaka kuondoa kinyesi hicho.

Shayo alisema hajawahi kumuona mwalimu huyo akimwingiza mgenindani ya nyumba hiyo badala yake alikua akimalizana nao nje ya chumba chake.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo