Makamu wa Rais Dr.Mohamed Gharib
Bilali amelaani vikali vitendo vya mauaji na kudhuru watu wenye ulemavu
wa ngozi yaani albino na kusema kuwa serikali inawasaka wahusika wa
vitendo hivyo na pindi itakapowakamata itahakikisha wanachukuliwa hatua
kali za kisheria ili iwe funzo kwa wengine.
Akizungumza kwa hisia kali katika maadhimisho ya siku ya Skauti
duniani Dr.Bilali amesema vitendo hivyo havivumiliki kamwe na vimekuwa
vikiitia doa Tanzania kwa kuonekana kuwa vinara wa imani potofu ya kuwa
viungo vya mwanadamu kuwa mtaji wa utajiri kitu ambacho hakipo katika
nchi yoyote ile Duniani.