Katika hali isiyo kuwa ya kawada
familia tatu zenye watu 16 katika kijiji cha Mikese mkoani Morogoro
wanalazimika kulala nje kwa siku saba mfululizo baada ya nyumba
wanazoishi kuwaka moto mara kwa mara na kuunguza thamani za ndani na
vyakula huku chanzo cha moto hakifamahamiki na kusababisha hofu
kwa familia hizo kutaka kuyakimbia makazi yao.
Blog hii ilifika katika familia hizo na kuona vitu mbalimbali
vilivyoungua moto vikiwemo vyakula nguo madaftari ya wanafunzi huku
wakinamama na watoto pamoja na wazee wakiwa nje ambapo wamesema katika
hali isiokua ya kawaidia moto huo huwaka zaidi ya mara tisa kwa siku
na wanajaribu kuuzima lakini chanzo cha moto huo hakieleweki ingawa
nyumba hizo hazina umeme wala nishati ya aina yoyote inayosabaisha moto
ambapo wamefananisha tukio hilo kama la miujiza na kuomba watu wenye
imani mbambali kufika na kufanya maombi katika nyumba hizo kwani
wanateseka kwa kushindwa kulala ndani.
Nao viongozi wa serikali yakitongoji cha lukole katika eneo la
tukio hilo mwenyekiti Ramadhani Shaban amekiri kuwemo kwa matukio ya
moto kuwaka katika nyumba hizo kwa siku saba mfululizo ambapo amesema
si tukio la kawaida najitihada wanazozifanya kama serikali ya kijiji
wameanza kuwatafuta wachungaji na mashekhe ili kusaidia kufanya
maombi katika nyumba hizo kwnai familia hizo zinaishi katika mazingira
magumu ya kulala nje kwa muda mrefu.