Mkazi wa Morogoro Andrew Chimulimuli ametangaza
kuuza figo yake kwa kwa kiasi cha sh. Mil 90 ili kukabiliana na ugumu
wa maisha na kama akitokea mteja akahitaji kupunguziwa gharama watafanya
mazungumzo.
“Nimeamua
kujitolea nafsi yangu ili nisaidie familia yangu kwa sababu mimi si
kitu kama sina fedha, ndiyo maana nimejitolea kutoa figo yangu nipate
fedha”—Andrew.
Kwa mujibu wa Takwimu za Wizara ya Afya
kuna wagonjwa 470,000 T’zania ambao figo zao zimeshindwa kufanya kazi
kabisa na wanahitaji upandikizaji.
Mkurugenzi wa taasisi ya Figo Tanzania Jaji Frederick Werema aliwahi kusema kuwa kitendo cha uuzaji wa figo ni kosa la jinai, ili kuuza ni lazima wahusika wafuate taratibu za kisheria.
Uchunguzi wa gazeti la Mwananchi ulionyesha kuwa wapo baadhi ya watu ambao wamekuwa wakiuza figo kiholela.
