JAMANI JAMANI JAMANI.....UGUMU WA MAISHA WAPELEKEA JAMAA HUYU WA MOROGORO KUTANGAZA KUUZA FIGO YAKE

Mkazi wa Morogoro Andrew Chimulimuli ametangaza kuuza figo yake kwa kwa kiasi cha sh. Mil 90 ili kukabiliana na ugumu wa maisha na kama akitokea mteja akahitaji kupunguziwa gharama watafanya mazungumzo.

Nimeamua kujitolea nafsi yangu ili nisaidie familia yangu kwa sababu mimi si kitu kama sina fedha, ndiyo maana nimejitolea kutoa figo yangu nipate fedha”—Andrew.

Kwa mujibu wa Takwimu za Wizara ya Afya kuna wagonjwa 470,000 T’zania ambao figo zao zimeshindwa kufanya kazi kabisa na wanahitaji upandikizaji.

Mkurugenzi wa taasisi ya Figo Tanzania Jaji Frederick Werema aliwahi kusema kuwa kitendo cha uuzaji wa figo ni kosa la jinai, ili kuuza ni lazima wahusika wafuate taratibu za kisheria.

Uchunguzi wa gazeti la Mwananchi ulionyesha kuwa wapo baadhi ya watu ambao wamekuwa wakiuza figo kiholela.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo