Serikali
imesema itawataja hadharani watu wote wanaodaiwa kujihusisha na wizi wa
dawa zinazonunuliwa na serikali kupitia bohari kuu ya madawa (MSD) ili
waweze kutambuliwa na wananchi, ambao wamekuwa wakichangia ukosefuwa
dawa katika vituo vya afya na hosipitali za serikali hapa nchini.
Hayo yamesemwa na katibu mkuu wizara ya afya na ustawi wa jamii, Dk
Dornald Mmbando wakati wa ukaguzi wa kituo cha afya kijiji cha Msoga
kilichopo Bagamoyo mkoani Pwani, ambapo amesema tatizo la dawa limekuwa
likiongezeka siku hadi siku kutokana na baadhi ya watendaji na watumishi
wa serikali wasio waaminifu.
Dkt Mmbando amesema kuwa, serikali imejipanga kukabilina na
magonjwa ya mlipuko kwa kutoa elimu kwa wananchi juu ya magonjwa mapya
yanayoibuka na kuitikisa dunia, ambapo amewaomba wanainchi kutoa taarifa
pale wanapo muona mtu mwenye dalili za ugonjwa wanaoutilia shaka
ikiwemo ugonjwa wa Ebola.
Mbunge wa jimbo la Chalinze mheshimiwa Ridhiwani Kikwete amisema
kuwa, tatizo la upotevu wa dawa katika zahanati na vituo vya afya katika
jimbo la Chalinze mkoani Pwani, ni kubwa kukilinganishwa na upatikanaji
wa dawa, jambo linalo athiri utoaji wa huduma za afya, na kuleta
manung'uniko toka kwa wanainchi wanapoenda kupata huduma kwenye vituo
vya afya na zahanati katika jimbo la Chalinze.