RIPOTI YA UCHUNGUZI KUHUSU MCHEZAJI KUFIA UWANJANI HII HAPA

Matokeo ya uchunguzi wa mwili wa mchezaji soka kutoka nchini Cameroon, Albert Ebosse aliyefariki nchini Algeria miezi minne iliyopita yamebaini aliuawa baada ya kuvamiwa na kupigwa katika eneo la kubadilishia jezi na wala hakuuawa kwa kupigwa na kitu katika kichwa chake kama ilivyokua imeripotiwa hapo awali.

Mchezaji huyo aliyekua alikiitumikia klabu ya JS Kabylie alifariki mwezi Agosti baada ya timu yake kufungwa.

Matokeo ya uchunguzi ulifanywa na serikali ya nchini Algeria yalibaini kwamba mchezaji huyo wa aliyekua na umri wa miaka 24 aliuawa baada ya kupigwa na kitu katika sehemu ya nyuma ya kichwa chake.

Lakini uchunguzi uliofanywa na mtaalam anayechunguza chanzo cha kifo kufuatia ruhusa iliotolewa na familia yake, umeonyesha kuwa kifo chake kimetokana na uvamizi wa kikatili dhidi yake katika eneo la kubadilisha jezi.

Wakati huo, waziri wa michezo nchini humo Algeria, Mohammed Tahmi alisema, Ebosse alifariki baada ya kupigwa na kitu katika kichwa, kisa hicho kilichosababisha klabu hiyo ya Kabylie kupigwa marufuku kwa miaka miwili katika mashindano yoyote ya barani Afrika na kulazimishwa kucheza michezo yake ya nyumbani bila mashabiki.

Lakini matokeo ya uchunguzi wa Andre Moune yamesema kuwa kulikuwa na mvutano wakati wa uvamizi huo, ambapo Ebosse alipigwa ngumi katika kichwa chake ilioathiri fuvu lake la kichwa.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo