WATOTO nane wamekutwa wameuawa kwenye nyumba moja katika mji wa Cairns eneo la Queensland kaskazini mwa Australia.
Polisi wa eneo la Queensland wanasema kuwa waliitwa kwenda kwenye nyumba hiyo baada ya ripoti kutolewa kwamba mwanamke mmoja alikuwa amejeruhiwa vibaya. Lakini ndani ya nyumba hiyo polisi waligundua maiti za watoto nane.
Inaaminika kuwa watoto hao walichomwa visu hadi kufa. Polisi wanasema kuwa mtoto mdogo zaidi kati ya watoto hao alikuwa na umri wa miezi 18 na mkubwa zaidi alikuwa na miaka 15.
Polisi wanasema kuwa mama huyo hajakamatwa lakini anawasaidia kwa uchunguzi. Waziri Mkuu wa Australia, Tony Abbott amekitaja kisa hicho kuwa uhalifu mbaya na pia kuzitaja habari hizo kuwa za kuvunja moyo.
Wanazungumza na watu kadhaa akiwemo mwanamume aliyeonekana karibu na nyumba hio asubuhi na mapema, ingawa hakuna mtu yeyote amekamatwa.
CHANZO: BBC