MAKUBWA...MBEGU ZA KIUME ZA WENYE VVU KUSAFISHWA ILI KUONDOA VIRUSI

Hakika teknolojia inazua mengi, hata yale ambayo hayakuwahi kufikiriwa na mababu zetu karne nyingi zilizopita. 

Hivi karibuni, wanasayansi wameweza kugundua namna ya kuzisafisha mbegu za kiume za mtu mwenye virusi vya Ukimwi na kuondoa virusi hivyo ili kumwezesha kutungisha mimba bila kumwathiri mwenza wake.,
Hii ni kwa wenza ambao mwanamume anaishi na VVU na mwanamke akiwa hana virusi hivyo.
Programu hiyo maalumu ijulikanayo kama SPAR, ilibuniwa ili kuwasaidia wenza hao kupata mtoto bila kumwambukiza mama na mtoto ambao mwanamume anaishi na VVU aweze kuzalisha.
Inafanyikaje?
Kisayansi, damu pekee si kipimo cha kuonyesha kuwepo kwa maambukizo ya VVU katika mwili bali hata katika majimaji ya mwilini.
Ogani zinazozalisha majimaji ya mbegu za kiume huathiriwa kwa namna ya pekee na VVU.
Daktari Bingwa wa Uchunguzi wa magonjwa, Henry Mwakyoma anasema kwa kawaida Virusi vya Ukimwi hupenda kukaa katika chembehai nyeupe(CD4).
“Kwa kawaida VVU haviishi katika mbegu za kiume. Lakini hupendelea zaidi kukaa katika CD4 au chembehai nyeupe za damu ambazo zipo katika damu na katika majimaji ya mbegu za kiume au semen,” anasema.
Anasema ndiyo maana inawezekana mwanamume mwenye VVU asimwambukize mwenza wake.
“Kama hana michubuko mwanamke anaweza asipate maambukizo, kwa kuwa majimaji ya mbegu za kiume yanakosa mahali pa kuingia,” anasema.
Hata hivyo, Dk Mwakyoma aliona kuna ugumu kuzisafisha mbegu za kiume na kuondoa majimaji yake yenye VVU, ili kuzipandikiza mbegu hizo ili zitungishe mimba kama unavyosema utafiti huo.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo