Sheikh Ali Mzee Comorian (pichani) amefariki dunia muda mchache
uliopita nyumbani kwake mtaa wa Kariakoo jijini Dar es salaam. Shughuli
za maziko zinafanyika hapo hapo nyumbani kwake.Habari ziwafikie ndugu, jamaa, marafiki na majirani popote pale walipo.
Maziko yatafanyika kesho Jumatatu saa nne asubuhi. Atasaliwa Msikiti wa Makonde na atazikwa katika Viunga vya Wangazija mtaa wa Bibi Titi Mohamed, Dar es salaam.
Mwenyezi Mungu ampe Kauli Thabit
Imetolewa na:
Abdulrahman S. I. Mbamba