Mafundi hao wamesema baada ya kubaini
kuwepo kwa chuma ambacho hawakukitambua waliamua kutoa taarifa Polisi na
Jeshi la Wananchi JWTZ, ambapo Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kigoma Jafari
Mohamed amethibitisha kutoa kwa tukio hilo.
Kamanda huyo amesema wanaendelea
kuwahoji watu kadhaa ikiwemo Diwani wa wa Kata hiyo ambaye alikuwa
anaimiliki nyumba hiyo kabla ya kuiuzia Halmashauri ya Wilaya ya
Kibondo, Mkuu wa Wilaya ya Kibondo Venance Mwamoto amesema huenda mabomu
hayo yaliachwa na wapiganaji wa kutoka Burundi walipokuwa nchini kama
Wakimbizi.