Watu wawili wamefariki dunia Wilayani Muleba baada ya kula ugali wa muhogo unaosadikiwa kuwa na sumu.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kagera Henry Mwaibabe alisema tukio hilo
lilitokea usiku wa kuamkia jana ambapo mama na mtoto wake walifariki
dunia huku ndugu wengine wanne wakiendelea kutibiwa hospitali.
Alisema familia hiyo ilinunua udaga kwa ajili ya kusaga unga na baada
ya kuutumia hali zao zilibadilika na kukimbizwa hospitalini ambapo mama
na mwanaye wa miaka mitano walifariki njiani kabla ya kufikishwa
hospitali.