WANAFUNZI WA CHUO KIKUU WAPINGA SHERIA INAYOWAZUIA KUPIGANA MABUSU

Muungano wa wanafunzi umelaani sheria mpya iliyopitishwa na uongozi wa chuo kikuu cha Zimbabwe ambayo inapiga marufuku wanafunzi hao ‘kupigana mabusu’.

Taarifa iliyoandikwa na shirika la utangazaji Uingereza BBC, imesema kiongozi wa muungano wa wanafunzi Zimbabwe, Gilbert Mutubuki amesema wataungana kuipinga sheria hiyo kandamizi inayowanyima uhuru na kuwafanya wanafunzi hao wa chuo kikuu kulinganishwa na watoto wa chekechea.

Katika vipeperushi vilivyobandikwa sehemu mbali mbali chuoni hapo, vimeandikwa amri kuwa yoyote atakayekutwa katika mazingira ya kutatanisha kama vile kupigana mabusu ama kufanya mapenzi hadharani ataadhibiwa vikali.
kIPEPERUSHI
Vile vile sheria hiyo imekataza wanafunzi kuwaingiza wenzao wa jinsia tofauti katika mabweni yao, pamoja na kuleta marafiki zao katika eneo la chuo ambapo wamesema ni sheria inayowanyima haki ya kujumuika na wenzao.

Wanafunzi wa vyuo vikuu nchini humo wamekuwa wakipingana na serikali mara kwa mara, ambapo kwa sasa kiongozi huyo wa wanafunzi amehimiza wanafunzi wenzake kuipinga sheria hiyo.
ZINASU


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo