Shahidi wa kwanza katika kesi ya kulawiti na kutuma picha katika
mitandao ya kijamii inayowakabili wakazi wawili wa Mbagala, ameieleza
Mahakama kuwa alikuwa na uhusiano wa mapenzi na mlalamikaji kwa kipindi
cha miaka saba, huku akiwa na mume wake ambaye ni mshtakiwa namba moja
katika kesi hiyo.
Shahidi huyo, Sanifa Sadick alidai mahakamani hapo
jana wakati akitoa ushahidi kuwa mshtakiwa, Erick Kasira (39) ni mume
wake tangu mwaka 2006 na wana watoto wawili.
Sanifa alisema kuwa Agosti 23 mwaka huu,
waliwasiliana na mlalamikaji ili wakutane nyumba ya kulala wageni ya
Maembe Bar & Guest House iliyopo, Yombo Kiwalani kwani alikuwa na
shida ya Sh100,000.
Shahidi huyo alidai kuwa wakati anaelekea eneo la
tukio kwa usafiri wa bodaboda, aliona pikipiki nyingine ikifuatilia kwa
nyuma hadi eneo hilo.
“Nilikuwa na shaka wakati pikipiki nyingine ikitufuatilia kwa nyuma,” alisema shahidi huyo katika utetezi wake.
Alidai kuwa alimkuta mlalamikaji peke yake na
kuagiza kinywaji, kabla ya kuchukua chumba namba sita na wakiwa ndani,
mlango wa chumba uligongwa na ndipo alimuona mume wake akiwa na vijana
watatu ambao hakuwafahamu.
Katika kesi ya msingi, washtakiwa wanadaiwa
kufanya vitendo vya ulawiti kwa mlalamikaji baada ya kushindwa kulipa
kiasi cha Sh1 milioni kama adhabu ya kukutwa na mke wa mtu.
Washtakiwa hao wanadaiwa kumlawiti Idd Kambi baada ya kushindwa kutoa Sh 1milioni kwa madai kuwa alikuwa na mahusiano ya kimapenzi na mke wa mmoja wa washtakiwa hao.
Washtakiwa hao wanadaiwa kumlawiti Idd Kambi baada ya kushindwa kutoa Sh 1milioni kwa madai kuwa alikuwa na mahusiano ya kimapenzi na mke wa mmoja wa washtakiwa hao.
Washtakiwa walimkuta mlalamikaji Kambi akiwa na
Sanifa Bakari katika chumba namba sita na hivyo kumshtumu kuwa
ana mahusiano ya kimapezi na mwanamke huyo kutokana na mshtakiwa mmoja
kudai kuwa ni mke wake na kwamba wamemfumania
Hata hivyo hakimu Mfawidhi wa Mahakam mahakama hiyo, Said Mkasiwa aliahirisha kesi hiyo hadi Novemba 3 mwaka huu itakapoendelea.
Na Hadija Jumanne
Na Hadija Jumanne