Wanafunzi
zaidi ya mia mbili hamsini na walimu zaidi ya kumi na tano wa shule ya
sekondari Mandewa iliyopo katika manispaa ya Singida haina vyoo,jambo
ambalo linawalazimu kuchangia katika choo cha kantini tokea shule hiyo
ilipoanzishwa mwaka elfu mbili na sita.
Wakieleza walimu na wanafunzi katika harambee iliyo itishwa na
shule hiyo kuchangia matatizo mbalimbali ikiwemo ujenzi wa maabara
wamesema ni jambo la aibu mwanafunzi kukutana na mwalimu katika choo
kimoja.
Akielezea changamoto katika shule yake mkuu wa shule ya sekondari Mandewa Bi. Magreth Misanga amesema ukosefu wa vyoo vya walimu katika
shule yake imekuwakero kwa walimu kwani ina walazimu kutumia choo kimoja
na wanafunzi.
Kwa upande wake mgeni rasmi katika harambee hiyo rais wa shirikisho la
wachibaji madini Tanzania Bwana John Bina, pamoja na kuwata walimu
wasivunjike moyo kufundisha amewachangia malori saba ya mchanga na
shilingi laki tano kwa ajili ya ujenzi wa vyoo ,ili kuondoa tatizo la
hilo la kuchangia choo wanafunzi na walimu.
Katika harambee hiyo zaidi ya shilingi laki saba mifuko ya saruji ishirini na tano pamoja na lori saba za michanga vimepatikana.