Kituo Kikuu cha Polisi cha Manispaa ya Lindi kimenusurika kuungua baada ya mlipuko kutokea wakati askari wakifanya usafi.
Tukio hilo lilitokea jana saa 1:30 asubuhi.
Imeelezwa kuwa askari hao walikuwa wakizichoma moto takataka ambazo zilikuwa na vitu vilivyolipuka.
Mlipuko ulikuwa na kishindo kikubwa kiasi cha kusababisha taharuki kwa watu waliokuwapo kituoni hapo na maeneo ya jirani.
Imeelezwa kuwa askari hao walikuwa wakizichoma moto takataka ambazo zilikuwa na vitu vilivyolipuka.
Mlipuko ulikuwa na kishindo kikubwa kiasi cha kusababisha taharuki kwa watu waliokuwapo kituoni hapo na maeneo ya jirani.
Kamanda wa polisi wa Mkoa wa Lindi, Renata Mzinga
alisema mlipuko huo ulisababishwa na chupa ambayo hata hivyo hakueleza
ilikuwa na kitu gani kinacholipuka.
“Kuna uharibifu umetokea. Vioo vya dirisha la
ofisi ya mkuu wa kituo na chumba cha mashtaka vimevunjika kutokana na
kishindo hicho,” alisema Kamanda Renata.
Awali, kabla Kamanda huyo hajatoa ufafanuzi,
taarifa zilizozagaa mitaa zilidai kuwa lilikuwa ni bomu linalotumiwa na
wavuvi haramu wa samaki.
Ilidaiwa kuwa lilikuwa limefichwa kwenye takataka zilizokusanywa nyuma ya kituo hicho.
Ilidaiwa kuwa lilikuwa limefichwa kwenye takataka zilizokusanywa nyuma ya kituo hicho.
Baadhi ya watu pia walidai kuwa mabomu hayo ya kienyeji hutupwa hovyo mitaani hivi sasa.