Jeshi la Polisi Tanga linamshikilia mtoto mwenye miaka 16 kwa kosa la
kunywa sumu kwa lengo la kujiua baada ya kunusurika kubakwa na baba yake
mzazi.
Kamanda wa Polisi Tanga Frasser Kashai alisema tukio hilo lilitokea
Oktoba 18 mwaka huu wakati baba yake Richard Leornad alipomvamia kwa lengo la
kutekeleza ubakaji huo lakini mtoto huyo alifanikiwa kumtoroka na
kuokolewa na wasamaria wema.
Alisema kwa sasa mtoto huyo anatibiwa katika hospitali ya Bombo chini
ya uangalizi wa Jeshi la Polisi huku baba yake huyo akishikiliwa na
Polisi kwa uchunguzi zaidi.