MAJONZI: JENGO LA TB JOSHUA LAPOROMOKA NA KUUA WATU

Watu kadhaa wanahofiwa kufariki mjini Lagos Nigeria baada ya jengo moja linalohusishwa na muhubiri mashuhuri nchini humo TB Joshua kuanguka.

Ripoti zinasema kuwa miili kadhaa imetolewa katika vifusi vya jengo hilo.

Shirika la kusimamia dharura nchini humo NEMA ,limesema kuwa jengo hilo ni la nyumba za kulala za wanachama wa kanisa la All Nations katika wilaya ya Ikotun.

Jengo hilo la ghorofa mbili lilikuwa likiongezwa ghorofa nyengine mbili lilipoanguka.

Maelfu ya watu mara nyingi uhudhuria maombi yanayoongozwa na TB Joshua anayejulikana kama mtume,kwa kuwa wanavutiwa na uwezo wake wa kuwaponya watu
 
CREDITS:BBC


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo