MADUKA KARIAKOO YAPIGWA MAKUFULI....NI KUSHINIKIZA KUGOMEA MASHINE ZA EFD

Baadhi ya maduka yaliyoko  mitaa mbalimbali ya Kariakoo yakiwa yamefungwa.

BAADHI ya wafanyabiashara wa Kariakoo jijini Dar es Salaam, wamegoma kufungua maduka wakidai warudishiwe mashine za mkono za awali badala ya zile za EFD, wakisema zinatumia ‘network’ na inapokuwa  haipo panakuwa na  usumbufu kwa wauzaji na wateja.

Kamera ya  GPL imezunguka maeneo mbalimbali ya mitaa ya  Kariakoo, na kujionea maduka yakiwa yamefungwa huku kukiwa hakuna wingi wa watu kama siku zingine.
Gabriel Ng’osha na Haruni Sanchawa/GPL


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo