Siku Kadhaa
zilizopita Madereva wa Bodaboda waliingiwa na hali ya wasiwasi kutokana
na matukio kadhaa yaliyotokea Mkoani Njombe dhidi yao na hivyo
kuhatarisha usalama wa kazi zao.
Madereva hao
wameonekana kuingiwa na hofu hiyo Ikiwa ni Wiki Moja tu Kupita Tangu
Dereva Mwenzao wa Bodaboda Wa kituo cha Eneo la Sangamela Mjini Njombe
Kutekwa na kuuawa Kinyama na Watu Wanaosadikika Kuwa ni Majambazi Ambapo
Mtu mmoja Aliyekodi Pikipiki Kwa Kijana Huyo Ndiye Anasadikika
Kusababisha Mauaji ya Dereva Huyo.
Sanjari na
Hilo Lakini Pia Hivi Karibuni Kijana Mmoja Ambaye Hakujulikana alikutwa
ametekwa na kutupwa Kwenye Maeneo ya Kata ya Njombe Mjini Ambaye
Inasadikika Kuwa naye Alikuwa Dereva wa bodaboda.
Kutokana na
matukio Hayo Madereva wa Bodaboda Mjini Njombe Wameingiwa na Hofu na
Kuanza Kufikiria Mbinu Mbalimbali za Kuweza Kujilinda Bila Kupata Majibu
ya Haraka.
Hivyo Jeshi
la Polisi Mkoani Njombe Kupitia Kitengo cha Usalama Barabarani
Limelazimika Kuwaita na Kujadili Namna ya Kuimarisha Ulinzi Katika
Biashara zao.
Picha na Michael Ngilangwa.