MAANDAMANO YA KULIFUNGA BUNGE MAALUM LA KATIBA YAJA

Jukwaa la Katiba Hapa nchini limeonya kuwa litahamisha maandamano ya wananchi kutoka sehemu mbali mbali nchini, kwenda kufunga ofisi za Bunge Maalumu la Katiba mjini Dodoma.

Hatua hiyo itafikiwa iwapo mwenyekiti wake Mh. Samuel Sitta hatasitisha vikao vya bunge hilo mara moja kutokana na kutokuwa na umuhimu kwa nchi hasa baada ya kufikiwa kwa muafaka baina ya vyama vikuu vya upinzania kwenye bunge la katiba.

Mwenyekiti wa Jukwaa hilo Bw. Deus Kibamba amesema hatua ya kutaka kufunga ofisi za Bunge Maalumu la Katiba inatokana na kile alichoeleza kuwa matumizi mabaya ya fedha za walipa kodi zinazotumika kwa matumizi yasiyo na tija.

Kwa mujibu wa Kibamba, kuendelea kwa bunge hilo hakuna mantiki yoyote hivi sasa ambapo pia Jukwaa limependekeza Sitta pamoja na mwanasheria Mkuu wa Serikali jaji Frederick Werema wasiruhusiwe kugombea nafasi yoyote ya kisiasa kwa kipindi cha miaka kumi kutokana na kile ilichodai kuwa ni kuhusika kwao katika kuvuruga mchakato wa katiba.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo