HIFADHI YA TAIFA YA KITULO MAKETE YAJIPANGA VILIVYO KUPAMBANA NA MAJANGILI WA ZAO LA CHIKANDA

Kutokana na zao la Chikanda linalopatikana katika hifadhi ya taifa ya Kitulo iliyopo Makete mkoani Njombe kuwa hatarini kutoweka, uongozi wa hifadhi hiyo umejipanga kikamilifu kupambana na waharibifu wa zao hilo. 

Kauli hiyo imetolewa na Kaimu mkuu wa hifadhi hiyo Bw. Pius Mzimbe katika mahojiano maalum na eddy blog iliyotembelea hifadhi hiyo kujua walivyojipanga kupambana na ujangili dhidi ya zao hilo. 

Bw. Mzimbe amesema zao hilo lipo hatarini kutowena kutokana na watu wasio waaminifu kuingia hifadhini humo bila kibali na kuanza kuchimba zao hilo la Chikanda ambapo licha ya kusababisha uharibifu wa zao hilo lakini pia wamekuwa wakiharibu mimea mingine pamoja na mazingira kwa ujumla. 
 Mkuu wa wilaya ya Makete Mh. Josephine Matiro (kushoto)akipata maelezo kuhusu zao la Chikanda.

"Lakini tu nikuhakikishie ndugu mwandishi tumejipanga vizuri, wapo watu ambao wamefungwa jela, wengine wamelipa faini na pia wapo ambao kesi zao zipo mahakamani, na sisi tumejipanga kuimarisha doria na ulinzi wa kutoka kuhakikisha watu hao hawaingii kwenye hifadhi na pindi wanapoingia basi wanadhibitiwa mara moja" amesema Mzimbe. 

Kwa hivi sasa kutokana na uchunguzi walioufanya wamegundua soko la zao hilo lipo nchi jirani hasa Zambia ambapo hutumia zao hilo kuandaa vyakula maalum kwa ajili ya sherehe, na kutokana na zao hilo kuwepo katika hifadhi ya Kitulo hulazimika kuuzwa kwa gharama kubwa. 

Kwa mujibu wa sheria za nchi ni kuwa zao la Chikanda ni nyara ya serikali hivyo hairuhusiwi kuchimbwa hata kama zao hilo lipo nje ya hifadhi hivyo kwa yeyote atakayekamatwa na zao hilo atachukuliwa hatua za kisheria kwa kukamatwa na nyara za serikali kinyume cha sheria, hivyo hifadhi hiyo kutoa wito kwa wananchi hasa wanaoizunguka hifadhi hiyo kutoa ushirikiano kuhakikisha rasilimali zilizopo hifadhini humo zinaendelea kuwepo na haziaribiwi na watu wasio waaminifu. 

Na Eddy Blog, Makete


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo