WAJUMBE WA KAMATI YA ULINZI NA USALAMA MAKETE WAGUSWA NA YATIMA MATAMBA NA KUWACHANGIA HELA

Wajumbe waliotembelea hifadhi ya taifa ya Kitulo wakiongozwa na kamati ya ulinzi na usalama ya wilaya ya Makete mkoani Njombe wameonesha kuguswa na kituo cha watoto yatima Fema Matamba na kuamua kuchanga fedha kwa ajili ya Kituo hicho. 
 
Wajumbe hao walichanga fedha zao kwa hiari ambapo walikabidhi kiasi cha tsh 138,000/= taslimu ambazo walizikabidhi kwa mlezi wa kituo hicho. 
 
Hatua hiyo inatokana na kituo hicho kinacholelea watoto yatima kuhitaji misaada kwa kuwa bado hakijaweza kuwa na miradi inayokiingizia kipato kiasi cha kuweza kulea watoto hao bila msaada wa watu mbalimbali. 
Fedha hizo zilikabidhiwa na afisa maliasili na mazingira Bw Uhuru Mwembe kwa niaba ya mkuu wa wilaya ambaye ni mwenyekiti wa kamati ya ulinzi na usalama wilaya ya Makete. 
 
Mlezi wa kituo hicho aliwashukuru kwa msaada huo na kusema kuwa wameonesha moyo wa kipekee na watalipwa na mwenyezi Mungu kwa kuwa ni jukumu la kila mmoja kusaidia watoto yatima kwa kadri atakavyojaliwa na mwenyezi Mungu
 
Na Eddy Blog, Makete


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo