POLISI WAANZA KUCHUNGUZA MAUAJI YA UTATA YA WANAWAKE WAWILI JIJINI ARUSHA




Kamanda wa Polisi Mkoani Arusha, Liberatusi Sabas, amesema jeshi lake lipo kwenye uchunguzi dhidi ya mauaji na kujeruhi wanawake Jijini Arusha, bila kuchukuliwa kitu chochote.

Amesema kwa sasa kumekuwepo na matukio mawili ya kuvamiwa kwa wanawake na kujeruhiwa kwa risasi, huku wahusika wakitokomea kusikojulikana bila kubeba kitu chochote.
 
Ametaja tukio la kwanza limetokea eneo la Kwa Iddi Sakina, ambapo Flora Porokwa alivamiwa na vijana wa pikipiki na kumfyatulia risasi na kumjeruhi akiwa ndani ya gari yake, kisha kutokomea.
 
Tukio la pili mwanamke mwingine, Samimu Rashidi (30), alivamiwa Agosti 6 mwaka huu, usiku saa 3 na kupigwa risasi ya shingoni na kufa akiwa ndani ya gari lenye namba T.569 BAY aina ya Toyota.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo