MAREKANI YAANZA KUWASAKA WALIOMCHINJA MWANDISHI WA HABARI




Kitengo cha sheria nchini ya Marekani kimeanza kufanya uchunguzi wa jinai dhidi ya kifo chamwandishi wa habari mwenye asili ya Marekani ,James Foley aliyeuawa na wapiganaji wa kiislamu wenye msimamo mkali.
 
Mwanasheria mkuu wa kitengo hicho,Eric Holder ameweka wazi kuwa wote waliohusika na mauaji ya mwandishi huo watawatia mkononi muda si mrefu.
 
Maofisa wa serikali ya Marekani wanadai kwamba askari hao wauaji walidai kiasi kikubwa cha pesa zipatazo dola za kimarekani zaidi ya milioni mia moja na thelathini kama fidia ya kumuachilia James Foley.
 
Marekani imekwisha anza harakati za kuwasaka na hatimaye kuwakamata waliohusika na mauaji ya mwandishi huyo kwa kurusha ndege zake takriban sita katika anga inayomilikiwa na waislamu kaskazini mwa Iraq.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo