HUYU NDIYO MAHABA NIUE WA MSANII DIANA KIMARO

Mastaa wa filamu nchini Diana Kimaro na Manaiki Sanga ni wapenzi. Juzi zilipenyezewa habari kuwa Manaiki anatoka na Diana Kimaro na kwasasa wameshibana vya kutosha kila mtu yupo hoi kwa mwenzake kama mlenda.

Uzuri ni kuwa wakati udaku huo ukipenyezwa Manaiki mwenyewe alikuwepo eneo hilo ambapo wasanii kadhaa walikuwa wakifuturu pamoja hivyo haraka sana tukampiga swali la moto Manaiki kama ni kweli yeye na Diana kwasasa ni honey, sweet na mpenzi? 
Manaiki alibaki kuangua kicheko ambacho kilitoa jibu la moja kwa moja kuwa hajiwezi kwa Diana ambaye kadri siku zinavyozidi kwenda ndivyo anavyozidi kujiimarisha kwenye tasnia ya filamu Swahiliwood.

Pia kupitia mitandao ya kijamii Manaiki amekuwa akiandika ujumbe na kupost picha akiwa na Diana. moja wa ujumbe huo ni huu:
 "#love #never #die japokua haupo na Mimi ila everyday mi naku feel baby sijuwi kupendwa kama we ulivyokua unanipenda na hiyo ni habari ya mjini"


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo