BREAKING NEWS..!! MTANGAZAJI WA REDIO MOSHI FM HENRY LYIMO "KIPESE" AFARIKI DUNIA KATIKA AJALI MBAYA USIKU HUU


  Marehemu Henry Lyimo enzi za Uhai wake
 
Kwa mujibu wa habari zilizotufikia hivi punde ni kwamba Mwandishi wa habari na Mtangazaji maarifu wa kipindi cha Michezo cha redio Moshi FM ya mkoani Kilimanjaro Henry Lymo maarufu pia kwa jina la Kipese amefariki dunia usiku huu.

Meneja wa Vipindi Redio Moshi FM Yusuph Mazimu amesema  mwili wa marehemu umehifadhiwa katika hospitali ya Kilema, Marangu Moshi.

Marehemu Henry Lymo mwenye tisheti nyekundu enzi za uhai wake akihojiwa na Mtangazaji wa sasa wa Kahama fm Halid Mchopa
 
Inasemekana Kipese amepata ajali ya pikipiki kwa kugogwa na gari wakati akitoka kuchezesha mechi ya mpira wa miguu maeneo ya himo mkoani Kilimanjaro.
 
Habari zaidi tutaendelea kuwaletea... Inalilah wainalilah rajuun.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo