skip to main |
skip to sidebar
ZIARA YA MBOWE YABAINI CHUMBA CHA DARASA WANACHOSOMEA WANAFUNZI CHAGEUZWA STOO YA KUNI HAI KILIMANJARO

Mbunge wa Jimbo la
Hai, Freeman Mbowe akishuhudia uharibifu kwenye moja ya madarasa ya Shule ya
Msingi Weruweru iliyoko wilayani Hai, ikiwa ni sehemu ya ziara yake anayofanya
pamoja na kamati yake ya Mfuko wa Maendeleo ya Jimbo (CDF), kwa ajili ya
kutathmini na kukagua miradi mbalimbali ya maendeleo jimboni kwake ili mfuko
huo uweze kusaidia kuongeza nguvu za ujenzi. Mbowe ambaye ni mwenyekiti wa
kamati ya mfuko huo alielezwa kuwa shimo hilo limekuwa likitumika na wananchi
waovu kama 'mlango' wa kuingia na kutoka kwa ajili ya kuiba kuni zinazotunzwa
katika chumba hicho cha darasa.

Mmoja wa Wanakamati wa
Kamati ya Mfuko wa Maendeleo (CDF) Jimbo la Hai akipanga kuni katika moja ya
madarasa ya Shule ya Msingi Shirimatunda iliyoko wilayani Hai, wakati
Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Freeman Mbowe (Mbunge wa Hai), alipofanya ziara ya
kukagua miradi mbalimbali ya maendeleo jimboni humo ambayo mfuko huo utasaidia
kuongeza nguvu za ujenzi. Chumba hicho mbali ya kutumika na wanafunzi kwa ajili
ya kusomea, pia kinatumika kama stoo ya kuni za kupikia chakula cha wanafunzi
shuleni hapo, hali ambayo inadhihirisha kuwepo kwa mahitaji ya vyumba kwa ajili
ya matumizi mbalimbali.
JIUNGE NA EDMO BLOG SASA
Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube
Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi