Wakili wake ameambia BBC kuwa mwanamke huyo aliyekiuka dini kwa kwa kuolewa na mwanamume mkristo aliachiliwa huru Jumatatu
Hukumu ya kifo iliyotolewa dhidi ya Meriam
Ibrahim,ilibatilishwa na mahakama ya rufaa, kwa mujibu wa shirika la
habari la Sudan Suna.
Meriam ameolewa na mwanamume mkristo na
alihukumiwa kifo na mahakama ya kiisilamu kwa kosa la kuasi dini, baada
ya kukataa kukana kuwa yeye ni mkristo.
Hukumu dhidi yake ilichochea viongozi wa kimataifa walioilaani wakisema inakiuka haki za binadamu.
