Watu wasiojulikana wanasadikika kuiba begi kubwa maeneo ya Sinza, Dar
es Salaam wakidhani begi hilo lina pesa na badala yake wakakutana na
chatu mkubwa walipolifungua.
Wakazi wa Sinza walimkuta chatu huyo katika daraja akiwa karibu na
sanduku hilo linaloaminika kuwa lilimbeba chatu huyo.
Inaelezwa kuwa
wezi hao walilitupa begi hilo na kutokomea pasipojulikana baada ya kuona
mambo yamekuwa ndivyo sivyo.