WATU WAWILI WANAOHISIWA KUWA NI MAJAMBAZI WAMEUAWA NA WANANCHI WALIPOKUWA WAKIPORA FEDHA BENKI UWANJA WA NDEGE DAR

Watu wawili wanaodhaniwa kuwa ni majambazi wakiwa katika jaribio la kutaka kupora fedha kwa mmoja wa wateja aliyekuwa ndani ya benki ya NMB tawi la uwanja wa ndege,wakiwa na pikipiki aina ya Boxer wameuawa na wananchi waliamua kujichukulia sheria mkononi,huku jeshi la polisi kanda maalumu ya Dar-es-Salaam likiwashikilia watu watatu  mmoja akiwa ni mganga aliyekuwa akiwatibu kwa nguvu za giza na kudai kuwapa nguvu.
 
Kamanda wa polisi kanda ya maalumu ya Dar-es-salaam,kamishana wa polisi Selemani Kova amesema kuwa,watuhumiwa hao wa ujambazi walipoteza maisha mara baada ya kipigo na kupoteza maisha wakiwa njiani kupelekwa hosipitalini,ambapo amesema katika tukio hilo walikutwa na bastola waliyotumia kurushiana risasi na polisi.

Jeshi la polisi limezitaka taasisi za kifedha kama mabenki na taasisi na watu binafsi kuacha mtindo wa kubebeba fedha kwa njia ya mifuko ya plastiki maarufu kama rambo,kubebea kwenye pikipiki na aina nyingine za usafirishaji fedha ambazo zinatoa vishawaisi kwa watu wasio na nia njema kuleta hujuma.

Baadhi ya wananchi walioshuhudia wamesema kuwa watuhumiwa hao walikuwa wakikimbia hovyo huku wakirusha risasi hewani, ambapo wamelishukuru jeshi la polisi kwa kudumisha doria na kulitaka jeshi hilo kushirikiana na wananchi ili kuhakikisha kuwa vitendo vya uporaji hasa kwenye  mabenki vinakomeshwa.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo