MTOTO WA MIAKA 7 AGONGWA NA GARI NA KUFARIKI DUNIA PAPO HAPO

MTOTO aliyefahamika kwa jina la Najma Benjamin (7) amefariki dunia papo hapo baada ya kugongwa na gari maeneo ya Bayuni Sheratoni, Kata ya Chanika, Wilaya ya Ilala jijini Dar es Salaam.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Ilala, Ally Omary Mnzava, amesema kuwa huko Barabara ya Chanika, gari aina ya Toyota Noah yenye namba T 611 CUN ikiendeshwa na Kasimu Ally (22) mkazi wa Chanika Mwisho, imemgonga mtembea kwa miguu ambaye ni mtoto huyo.

Mnzava amesema mtoto huyo amefariki dunia papo hapo baada ya kugongwa na gari, ambapo dereva kwa sasa amekamatwa na maiti kuhifadhiwa katika Hosptali ya Taifa Muhimbili huku upelelezi ukiendelea.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo