LORI KUVUNJA DARAJA LA TABATA SEGEREA WANANCHI WATOA MAONI YAO

Wakazi wa Tabata Kinyerezi wamekosa mawasiliano na maeneo mengine ya jiji baada ya lori lililobeba tani arobaini kutumbukia kwenye daraja la Segerea lenye uwezo wa kupitisha tani saba .

Lori hilo likiwa limebeba matofali na kudaiwa kuwa na abiria sita ambao wawili wanasemekana kupoteza maisha na wanne wakiwa wamejeruhiwa vibaya baada ya dereva kukatazwa kupitisha lori hilo lenye tani 40 ambapo kibao kinaonyesha tani 7.

Wananchi wa Kinyerezi wameiomba serikali kumchukulia hatua kali dereva huyo ambae amesababisha hasara kubwa ya miundombinu ya serikali licha ya kukatazwa na wakandarasi .

Mkandarasi wa daraja hilo amekiri kutokea kwa ajali hiyo na wanachokifanya sasa ni kuweka daraja la muda ili wananchi waweze kupita.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo