HALMASHAURI YA MJI MDOGO WA MOMBO KULA SAHANI MOJA NA ABIRIA WANAOTUPA TAKA NJE WAKIWA NDANI YA MABASI

Halmashauri ya mji mdogo wa Mombo imetunga sheria ndogo ya kuwabana wenye mabasi kudhibiti abiria wao wasitupe taka hovyo hasa za mabaki ya vyakula wanapaokuwa katika maeneo ya miji ili kuepuka uchafuzi wa mazingira unaofanywa na baadhi ya wasafirishaji na kuhatarisha afya za wakazi wa maeneo yaliyopo pembeni mwa mji huo.
 
Akihutubia wakazi wa mji mdogo wa Mombo katika zoezi la usafi wa kujitolea uliofanywa na kikundi cha Fahari Sanaa Group cha mji mdogo wa Mombo,mwenyekiti wa mamlaka ya mji huo Bwana Richard Luizile (PICHANI)amesema ameshatoa taarifa kwa afisa afya kuwaita mawakala wa kampuni za magari ya abiria kwa ajili kuwapatia wenye mabasi nakala ya sheria hiyo ambayo inaagiza kuwa kila mwenye basi lazima awe na chombo maalum cha kuhifadhia taka.
 
Amesema endapo baadhi ya abiria ambao watabainika kutupa taka hovyo kupitia dirishani hasa anapokuwa katika maeneo ya miji wahusika wa chombo cha usafiri watatozwa faini ya shilingi 50,000/= kila basi litakalobainika kukiuka sheria hiyo kwa  abiria wake kutupa taka hovyo watahakikisha wanawadhibiti watuhumiwa kupitia askari wa jeshi la polisi waliopo katika njia kuu ya kwenda mikoa ya kilimanjaro na Arusha ili kuhakikisha kuwa suala la uchafuzi wa mazingira linadhibitiwa. 
 
Kwa upande wake mratibu wa usafi wa maji mdogo wa mombo ambaye ni mwenyekiti wa taasisi ya Fahari Sanaa Group Bwana Hamis Ngota amesema suala la usafi halibagui itikadi,vikundi wala mkubwa kwa mdogo na badala yake ni kazi ya kila mmoja anapaswa kuzingatia sheria na taratibu za usafi katika eneo lake.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo