WIVU WA MAPENZI WASABABISHA MAUAJI HUKO MBEYA, MUME DAIWA KUUA MKE

Mwanamke mmoja  aliyetambuliwa kwa jina la Christina Hayola(35), mkazi wa Kijiji cha Lwalanje wilaya ya Mbozi mkoani Mbeya, amekutwa amekufa na mwili wake kubainika kuwa ulikuwa na majeraha ya kukatwa katwa Kifuani, kichwani na mguu wake wa kulia.
 
Unyama huo unadaiwa kufanywa na mumewe, Mussa Nsagaje, maarufu kwa jina la Mwaulambo.

Sababu za mauaji hayo zinatokana na kile kinachodaiwa kuwa  ni ugomvi wa masuala ya wivu wa kimahusiano(Ngono) ulioanzia eneo la kilabu cha pombe.
 
Mwili wa marehemu ulikutwa katika Kijiji cha Magamba, kata ya Isansa, tarafa ya Igamba, wilayani Mbozi, mkoani Mbeya na mtuhumiwa alitoroka baada ya kutekeleza mauaji hayo.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright 2025 EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo