Mratibu
wa kuthibiti ukimwi halmashauri ya manispaa ya iringa sekta ya
afya BONAVENTURA KALUMBETE amewataka wananchi wa manispaa ya iringa
kuendelea kujitokeza kwa wingi katika upimaji wa virusi vya ukimwi ,
magojwa ya zinaa, na katika huduma ya tohara.
KALUMBETE amesema kuwa ameridhishwa na mwitikio wanao uonyesha kwa kujitokeza kwa wingi katika upimaji wa magonjwa hayo.
Mratibu
huyo ameongeza kuwa waliojitokeza kupima virusi vya ukimwi mwezi
uliopita jana ni 2,541,na waliojitokeza kupima magonjwa ya zinaa
ni 306 wakati waliojitokeza kupata huduma ya tohara ni 356 hali
inayoonesha kuwa elimu juu ya uthibiti wa magojwa ambukizi imeenea
mkoani hapa.
KALUMBETE amesema
mkoa wa iringa umefanikiwa kupunguza maambukizi ya virusi vya ukimwi
kutoka nafasi ya kwanza kitaifa kwa asilimia 15.7 mwaka 2007/2008 hadi
kufikia nafasi ya pili kwa sasa ikiwa na asilimia 9.1 wakati nafasi ya
kwanza ikishikiliwa na mkoa wa njombe kwa asilimia 14.8.
Aidha amewataka vijana kuwa na tabia ya kupima afya kabla ya kuanza mahusiano .
