WAFANYABIASHARA WALIOVUNJIWA MEZA ZAO WAKATI WA OPARESHENI SAFISHA JIJI DAR, WAREJEA KWA KASI




Ikiwa imepita miezi kadhaa tangu halmashauri ya jiji la Dar kuendesha operesheni safisha jiji katika maeneo mbalimbali ikiwemo Posta, na kuwaondoa wale wote wanaofanya biashara kwenye maeneo hayo hivi sasa wafanyabiahsra hao wamerejea kwa kasi

Hii leo mpigapicha wa Eddy Blog amepita Posta jijini humo na kushuhudia biashara zikiendelea kwa kasi ikiwemo za uuzaji wa magazeti na biashara nyinginezo ambazo askari wa jiji walivunjavunja meza za kuuzia magazeti wakati wa utekelezaji wa operesheni

Mara nyingi kumekuwa na utaratibu wa kuanzisha operesheni ambapo baada ya muda mfupi wafanyabiashara hao hurejea baada ya kuona ulegevu wa muendelezo wa mambo hayo

Habari/picha na Eddy Blog Team


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo