VURUGU ZATOKEA NDANI YA KANISA ARUSHA, FFU WAMUOKOA ASKOFU ASIPIGWE




Askofu  mkuu  wa  kanisa  la  PEFA  Moivaro, lililopo  Wilayani  Arumeru, mkoani  Arusha, Charles  Nkya, juzi  amenusurika  kupigwa  na  waumini  wake  kanisani  baada  ya  kuibuka  vurugu  kubwa  ya  kugombea  madaraka....

Vurugu  hizo  zilitulizwa  na  askari  wa  kutuliza  vurugu  FFU, waliokuwa  na  silaha  za  moto  pamoja  na  mabomu  ya  machozi  ambao  walimuokoa  askofu  huyo...

Hali  hiyo  ilitokana  na  baadhi  ya  waumini  kukerwa  na  kitendo  cha  Askofu  Nkya  kuwabadilishia  mchungaji  wasiyemtaka  na  kutangaza  kuwatenga  baadhi  ya  waumini  kwa  madai  ya  kunuka  dhambi...

Tukio  hilo  lilichukua  zaidi  ya  saa  sita  hadi  kutulizwa  kwake  ambapo  waumini  waligoma  kuingia  kanisani  baada  ya  kupata  taarifa  kuwa  askofu  wao  alitaka  kubadilisha  uongozi  wa  kanisa  hilo  na  kumwondoa  mchungaji  wao, mama  Nai  Solomoni

Kabla  ya  muda  wa  ibada  kufika,waumini  waliofika  kanisani  hapo  mapema  walipigwa  na  butwaa  baada  ya  kukuta  kanisa  hilo  limevunjwa  mlango  wa  kuingilia  hivyo  kuzua  hofu  ya  kutegwa  mabomu...

Waumini  hao  walilazimika  kuita  polisi  toka  kituo  cha  polisi  Usa  River    ambao  walifika  kanisani  hapo  kufanya  upekuzi  na  kubaini  hakukuwa  na  dalili  zozote  za  kutegwa  bomu, hivyo  baadhi  yao  waliingia  kanisani.....

Hata  hivyo, waumini  wengine  waligoma  kuingia  kanisani  wakishinikiza  askofu  Nkya  kutofanya  uteuzi  wowote  wa  mchungaji  lakini  askofu  huyo  alishinikiza  na  kutangaza  kumteua  mchungaji  , Hyness  Munuo  ambaye  ni  mke  wa  mwanzilishi  wa  kanisa  hilo, marehemu  mchungaji  Elibariki  Munuo.....

 Mbali  na  uteuzi  huo, askofu  Nkya  alitangaza  kuwafukuza  baadhi  ya  waumni  aliodai  wanamuunga  mkono  mchungaji Solomoni  ambapo  hatua  hiyo  iliibua  vurugu  kubwa  kwa  baadhi  ya  waumini  ambao  walimjia  juu  askofu  wao  na  kuanza  kumshambulia  kwa  matusi, wengine  wakimtupia  viti  vya  kukalia  wakitaka  warudishiwe  fedha  walizochangia  ujenzi  wa  kanisa  hilo.....

Kutokana  na  vurugu  hizo, polisi  walipata  taarifa, wakafika  eneo la  tukio  na  kuwaweka  chini  ya  ulinzi  baadhi  ya  waumini  na  kumtaka  askofu  huyo  na  wasaidizi  wake  kuripoti  kesho  katika  kituo  cha  polisi  cha  Usa  River  ili  hatua  zaidi  ziweze  kuchukuliwa....

Mkuu  wa  upelelezi  wilayani  humo, OC CID  Jumanne  Mkwawa, alimtaka  askofu  Nkya  kusitisha  mabadiliko  ya  uongozi  wa  kanisa  hilo  kama  alivyotangaza  hadi  hapo  mwafaka  utakapopatikana


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo