Na Anna Nkinda – Maelezo
Wilaya
ya Kinondoni kwa kushirikiana na ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam
wanaandaa mkakati wa kusafirisha wanafunzi kwa vitambulisho maalum vya
wanafunzi kwa bei naafuu kwa kutumia mabasi ya UDA kwenda shule za
pembezoni.
Hayo
yamesemwa hivi karibuni na Afisa Elimu Sekondari wilaya ya Kinondoni
Omath Sanga wakati akisoma taarifa ya Idara ya Elimu kwa Mke wa Rais
Mama Salma Kikwete alipoitembelea shule ya Sekondari ya Kata ya Salma
Kikwete iliyopo Kijitonyama wilayani humo.
Sanga
alisema wanafunzi hao ambao wanatumia usafiri wa mabasi zaidi ya moja
kwenda shule kwa siku kutoka majumbani kwao kuelekea maeneo ya Goba,
Fahari, Kinzudi, Mabwe, Kisauke, Njechele, Mabibo, Malambamawili,
Hondogo, Gogoni, Kibwegere na Kibweheri mara baada ya kukamilika kwa
vitambulisho bivyo watalipa nauli ya shilingi 200 kwenda na 200 kurudi.
