WASANII nyota wa vichekesho Bongo, Ulimboka Mwalulesa ‘Senga Kijumule’
na swahiba wake, Yusuph Kaimu Machoti ‘Pembe’ hivi karibuni walifunga
mtaa mjini Kahama baada ya mashabiki kuwazunguka kwa dakika 45
wakiwashangaa.
Wawili hao ambao walijipatia umaarufu mkubwa wakati walipokuwa wakiigiza
kupitia televisheni, walikuwa katika Wilaya za Mbogwe na Kahama wakati
wa uzinduzi wa albamu ya tatu ya msanii wa muziki wa asili wa Kabila la
Wasukuma aitwaye Bhudagala.
Baada ya wananchi kuwaona wasanii hao wakitembea kwa miguu katika mitaa
mjini hapa, walianza kuwafuata taratibu na hatimaye kujikuta wakiwa
kundi kubwa ambalo halikutarajiwa.
