SPIKA MAKINDA AWAAGIZA WABUNGE WALIOCHUKUA POSHO BILA KUSAFIRI WAZIRUDISHE MARA MOJA

Sakata la baadhi ya wabunge kutuhumiana kuwa wamechukua fedha za serikali kwa ajili ya kufanya  Safari na hawakusafiri limechukua sura nyingine baada ya spika wa bunge Mh. Anne Makinda kuwataka  wale wote waliochukua fedha hiizo bila ya kusafiri wazirudishe na huku akisisitiza anawajua wote kwa majina.

Mh Makinda ameyasema hayo alipokuwa akiongoza mkutano wa kumi na nne na kikao cha kumi na tisa  ambapo amesema anashangazwa na maneno maneno ambayo wabunge wamekuwa wakitupiana  wakati anawajua wote waliochukua fedha bila ya kusafiri.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo