Mwili wa Adam Kuambiana ukiandaliwa tayari kwa kuagwa nyumbani kwake Bunju B jioni hii.
Waombolezaji
wakiwa msibani tayari kuaga mwili. Wa tatu kutoka kulia waliokaa mbele
ni mke wa marehemu Janeth Rithe ambaye ni Diwani Kata ya Kunduchi, Dar.
Watangazaji Sauda Mwilima (kulia) na Zamaradi Mketema (kati) wakiwa msibani hapo. Kushoto ni msanii Shamsa Ford.
William Mtitu (katikati) akiwa na waombolezaji.
Ibada ya kumuombea marehemu ikiendelea.
Mwili wa marehemu Adam Kuambiana ukitolewa kwa ajili ya kuagwa.
Baadhi ya wasanii baada ya kuwasili Bunju B.
Mwili wa marehemu ukiwasili nyumbani Bunju B.
Mwili wa marehemu ukishushwa kutoka kwenye gari Bunju B.
MWILI wa mwongozaji na mwigizaji wa filamu Bongo, Adam Kuambiana
umeagwa nyumbani kwake Bunju B, Dar ambapo ndugu, jamaa, wanasiasa,
marafiki wameshiriki tukio hilo. Kesho asubuhi mwili utapelekwa Viwanja
vya Leaders kuagwa na baadaye kuzikwa katika makaburi ya Kinondoni
jijini Dar.
(PICHA NA GABRIEL NG'OSHA, MAYASA MARIWATA, SHANI RAMADHAN / GPL)
JIUNGE NA EDMO BLOG SASA
Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube
Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi